Makala hii inahusu matapo na namna yanavyojitokeza katika fasihi simulizi. Fasihi ni sanaa inayotumia lugha na vitendo kuwasilisha ujumbe kuhusu maisha ya binadamu. Fasihi simulizi ndiyo fasihi mama na iliyo na historia ndefu. Hata hivyo, wataalamu wengi wamekuwa wakishughulikia dhana ya matapo katika fasihi andishi bila kuzingatia uwepo wa matapo katika fasihi simulizi ya Kiswahili. Makala inalenga kuyaweka wazi matapo ya fasihi simulizi ya Kiswahili ili kubaini mchango wake katika Sanaa. Vilevile, Makala yanalenga kutathmini matapo hayo kwa kutumia mifano kutoka katika mazingira halisi ya jamii. Utafiti ulifanywa kwa kutumia mbinu ya kiethonografia iliyohusisha kushiriki, kushuhudia na kuhoji pamoja na udurusu wa nyaraka zilitumika katika kukusanya nyimbo na vipengele mbalimbali vya fasihi simulizi katika kila tapo au kipindi. Nadharia ya Ujumi wa Kinudhuma na ile ya Wigo au Uigaji (Ethnopoetics and Emic Theory) ndizo zilizotumika katika kufanikisha utafiti huu. Uchanganuzi wa data na matokeo ulifanywa kwa kutumia mkabala wa kitaamuli. Makala hii imedhihirisha kuwa matapo yaliyopo katika fasihi andishi; Usasa na Usasaleo, ndiyo hujulikana kama Ukale na Ujadi katika fasihi simulizi ya Kiswahili. Aidha, makala imependekeza kufanyika kwa tafiti nyingine mbalimbali katika fasihi simulizi