Makala hii inafafanua na kujadili mofolojia isoshikanisho katika Kiswahili na dhana ya mofimu. Baada ya kuelezea sifa bainifu za mofolojia mshikanisho na isoshikanisho, mifano kadha ya mofolojia hiyo katika Kiswahili inafafanuliwa. Mifano hiyo ni katika vionyeshi, uradidi, na ufupishaji wa majina na nomino. Violezo na ruwaza vinaelezwa kuwa muhimu katika fasili ya mofimu katika mofolojia isoshikanisho. Makala inabainisha mofimu za Kiswahili zinaundwa na vipandesauti na violezo. Kwa upande mwingine, violezo hivyo na mifano ya vifupisho vya majina kuwa silabi mbili inabainisha dhima kubwa ya arudhi na katika kuunda maneno ya Kiswahili